ZAWADI NA NYUMBA ALI SEHEMU YA TATU NA YA MWISHO.

Hii ni sehemu ya mwisho katika simulizi ya Zawadi na Nyumba Ali ambapo nitaelezea shirika lilivyo nisaidia ili kutimiza ndoto zangu. Kama nilivyo eleza katika sehemu ya kwanza kuwa nilianza kuhudumiwa na Nyumba Ali mnamo mwaka 2009, kabla sija anza kuhudumiwa na Nyumba Ali nilikuwa mtu ambaye sina matumaini yoyote.

Nyumba Ali imenisaidia kusoma kuanzia darasa la kwanza mbaka sasa nimemaliza kidato cha nne, nakili wazi bila msaada wa Nyumba Ali nisingeweza kutimiza ndoto hiyo ya kusoma hadi kidato cha nne kwani wao walitambuwa kwamba ninao uwezo wa kusoma licha ya ulemavu nilionao. Natambua kuwa mtatamani kujuwa baada ya kuwa nimemaliza kidato cha nne nitaelekea wapi hii ni simulizi nyingine ambayo itakujia wiki ijayo hapahapa kwenye blog hii.

ENDELEA KUFWATILIA BLOG HII KWA MAENDELEO CHANYA KWA WALEMAVU TANZANIA.


MAADA YA WIKI:Wanawake wana mchango gani katika kuhakikisha haki za walemavu zinapatikana?

Unaweza kuchangia mada hii hapohapo kwenye blog au kupitia zawadimsigala1@gmail.com.

Pia unaweza kuomba ushauri kuhusu watu wenye ulemavu kupitia hiyo hapo juu


Maoni

  1. Zawadi, this is a very interesting topic. I think that disability is much more understood by women. So they must have all the support to study and work in this field. It is well known that also the volunteers in this field are mostly women. Much has to be done to involve also men. What do you think? What is your experience?

    JibuFuta
    Majibu
    1. Hi Zawadi, how are you? Do you like your studies ? I saw you many years ago in Bologna. Sorry for my terrific English.
      I hope that you came back in Italy, soon or later.
      Marina

      Futa

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii