ZAWADI NA NYUMBA ALI.

 

      Nyumba Ali ni shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na kulea  watoto wenye ulemavu katika manispaa ya Iringa. Shirika hili lilianzishwa mwaka 2007 na raia wawili wa kitaliano ambao ni bi Bruna na bwana Lucio. Sababu za kuanzisha nitazieleza hapo baadaye.  Huduma zitolewazo na shirika hili ni pamoja na mazoezi ya viungo, huduma za afya kwa watoto wenye ulemavu, wenye shida za kiafya, lishe bora kwa watoto wenye ulemavu, huduma ya makazi  kwa watoto  wenye ulemavu wenye mazingira magumu, huduma ya elimu kwa watoto wenye uwezo wa kusoma na huduma ya kuwapa elimu ya ufundi stadi kwa watoto wasio na uwezo wa  kusoma.

   Zawadi Msigala ambaye pia ni mmiliki wa jukwa hili ni kijana ambaye ninajivunia mafanikio makubwa ya kielimu licha kuwa ni mtu mwenye ulemavu. Mafanikio haya nimeyapata kutokana na msaada mkubwa wa shirika la Nyumba Ali, nilianza kuhudumiwa na shirika hili mwaka 2009.

                USIKOSE MUENDELEZO WA SIMULIZI HII.

MADA YA WIKI: Je, watu wenye ulemavu nchini Tanzania wanapewa haki zao ipasavyo?

Unaweza  kuchangia mada hii hapohapo kwenye blog au kupitia zawadimsigala1@gmale.com.

Pia unaweza kuomba ushauri kuhusu watu wenye ulemavu kupitia hiyo hapo juu

Maoni

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii