ZAWADI NA NYUMBA ALI SEHEMU YA 2.

     Katika sehemu ya kwanza nilisema kuwa sababu za kuanzish shirika nitazieleza hapo baadaye, sasa naomba niwaeleze sababu za kuanzisha shirika la nyumba Ali. Bi Bruna na Bwana Lucio walifika hapa nchini Tanzania kwa mara ya kwanza mnamo mwaka  2006 kwa lenngo la kupata mapumziko.  Baada ya kufika  hapa nchini walikuta changamoto kubwa ya watoto wenye ulemavu, waliguswa sana na changamoto hizo ndipo walipo rudi nyumbani kwao Italia walianza kuunda shirika la nyumba Ali huku wakiwa na lengo la kuwasaidia  watoto wenye ulemavu nchini, bila shaka changamoto za watoto wenye ulemavu ndizo sababu za kuanzisha shirika hili.

   Mimi kama Mtanzania ambaye pia ni mnufaika wa shirika hili nawapongeza na kuwashukuru Bi Bluna na Bwana Lucio kwa kuanzisha shirika hili ambalo limekuwa msaada mkubwa kwetu watu wenye ulemavu nchini.

Sehemu ya tatu itaelezea namna gani shirika limenisaidia mimi Zawadi Msigala.

                USIKOSE SEHEMU YA TATU YA SIMULIZI HII.

 

MADA YA WIKI: Nini kifanyike kwa  vijana wenye ulemavu ili waishi kama vijana wengine?

Unaweza  kuchangia mada hii hapohapo kwenye blog au kupitia zawadimsigala1@gmail.com

Pia unaweza kuomba ushauri kuhusu watu wenye ulemavu kupitia hiyo hapo juu

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii